Friday, April 18, 2014

Irene Uwoya Kufunga Upya Ndoa Ya Kifahari Na Tajiri Wa Madini Mwenye Pesa Za Kumwaga.

Irene Uwoya
Baada ya kudaiwa kutengana na aliyekuwa mumewe yaani Ndikumana Katauti toka nchini Rwanda, Star mkubwa wa filamu Swahiliwood Irene Uwoya anadaiwa kuwa katika mishe mishe za kufunga ndoa na jamaa mmoja mfanyabiashara wa Madini mwenye pesa zake ambaye anaishi Sinza, Dar es salaam. Habari zaidi zinadadavua kuwa jamaa huyo ameoza kwenye penzi la Uwoya ambaye alifunga ndoa ya kifahari na Ndikumana miaka michache nyuma na kuishia kuwa katika gogoro la mara kwa mara. Jamaa ndiye anataka kumuoa Uwoya haraka iwezekanavyo huku mashosti wa Uwoya wakimshangaa star huyo kama ataiweza ndoa hiyo baada ya kushindwa kwa Ndiku. "Inashangaza sana kwasababu hata Uwoya mwenyewe anaridhia hicho kitu, sasa sisi mashosti zake tunajiuliza alishindwa nini kwa Ndiku mpaka leo hii atake kuingia kwenye ndoa mpya?" Chanzo kililiambia gazeti la Visa

Chanzo hicho kilizidi kumwaga habari kwa kusema "huyo kijana kadata na Uwoya kwa kweli, hasikii la bibi yake wala la shangazi zake, kaamua na yeye ndiye kiherehere kutaka kumuoa Uwoya, na hizo pesa zake ndizo zinazomzuzua hata Uwoya mwenyewe"

Mashosti hao wa Uwoya walimalizia kwa kusema kuwa hata hivyo Uwoya atakuwa na wakati mgumu kwani mpaka sasa wazazi wake hawajui kuhusu issue hiyo ya ndoa mpya kwasababu wao ni waaminifu kwa dini yao ya kikiristu na pia bado wanamtambua Ndikumana kama mkwe wao kwasababu ndoa za kikiristu huwa hazivunjiki.

                                                                Uwoya
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Filamu kali ya SIO SAWA inaingia sokoni tarehe 24 April 2014 hakikisha unanunua nakala yako halisi.
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment