Sunday, July 20, 2014

Mtunisy Adaiwa Kumvisha Pete Ya Uchumba VJ Penny Kwa Siri Kubwa, Penny Avaa Ushungi Akubalike Ukweni !

VJ Penny na Mtunisy
Latest buzz is about Mtunisy kumvisha pete ya uchumba VJ Penny hivi juzi kati. Kwa mujibu wa chanzo kimoja kilicho karibu na Penny kikizungumza na Swahiliworldplanet. kilisema kuwa Mtunisy amemvisha Penny pete hiyo kwa siri kubwa na wamekuwa karibu kwa muda sasa bila hata watu wao wa karibu kujua. Habari zaidi zinadai kuwa Penny yupo tayari kuolewa na Mtunisy kama mke wa pili ndiyo maana kwa muda sasa amekuwa akivaa ushungi licha ya kuwa mkiristu ili akubalike ukweni ambapo Mtunisy ni muislamu.


"Mtunisy kamvisha VJ Penny pete ya uchumba mna taarifa? ilitokea hivi juzi walifanya siri sana hata mimi nilijua baadaye, wapo karibu siku hizi hata Penny anavaa ushungi ili akubalike kwa wakwe zake, Penny amechoka na upweke tangu aachane na Diamond"

Baada ya kupata habari hizo juzi ilibidi kumsaka VJ Penny ili atolee ufafanuzi hata hivyo juhudi ziligonga mwamba lakini Mtunisy alipatikana na alipoulizwa kuhusu kumvisha pete ya uchumba VJ Penny aling'aka na kusema hata hana namba ya Penny walikutana kikazi wakati wa kushuti kipindi kipya cha TV cha VJ Penny "Dah huo ni uzushi tu hakuna kitu Kama hicho hata namba ya huyo mtu sinayo nilikuwa Nae kwenye kipindi cha Bongowwod tu"

Siku chache zilizopita VJ Penny aliweka picha Instagram akiwa amevaa pete ya uchumba lakini hakutaja mwanaume ambaye amemvisha pete hiyo kiasi cha wafuatilia habari za mastaa kuanza kumfuatilia Penny kujua anatoka na nani.

                                                               Mtunisy
Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment