Tuesday, December 16, 2014

Diamond Platnumz Amsifia Shilole Huku Akimtupia Dongo Wema Sepetu Kiana !

Shilole, Diamond and Wema Sepetu
Superstar Diamond Platnumz ameandika ujumbe huo hapo chini kumsifia na kumpa moyo Shilole huku katika ujumbe huo baadhi ya mashabiki kuhisi kuwa amemtupia dongo kiana ex-girlfriend wake Wema Sepetu. Diamond aliweka kava la wimbo mpya wa Shilole na kuandika........

"Moja ya mfano mzuri tulionao Nchini...wakati anaanza kila mtu alimdharau na kumuona hatofika popote lakini leo hii Huwezi kusikia show kubwa inafanyika Nchini bila yeye Kuwepo...Dada zangu msikubali kuishi maisha ya kutegemea, Mbona mkijiamini wenyewe mnaweza... hivi hadi lini mtanyanyasika na Kuporwaporwa vitu baada ya Mahusiano kufa..Amkeni sasa! #Sio_wanaake_woteHuu mzigo wake mpya #MALELE @shilolekiuno"

No comments:

Post a Comment